Mbunge wa Singida Mashariki kupitia chama cha Chadema na mnadhimu mkuu wa upinzani Tanzania Tundu Lissu ametangaza kwamba atarudi nchini humo tarehe saba mwezi wa tisa ikiwa ni miaka miwili tangu aliposhambuliwa.
Akizungumza kwa njia ya simu na kupitia runinga ya Chadema mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe katika makao makuu ya Chadema Lisu amesema kuwa atarudi nchini Tanzania siku hiyo ili kuadhimisha kushambuliwa kwake.
''Nitatua tarehe saba mwezi septemba 2019 kwenye ardhi ya tanzania kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa nitakuwepo, alisema Tundu Lissu
No comments:
Post a Comment