Saturday, May 25, 2019

Huawei Kutangaza Vita na Kampuni ya IPhone kwa Kutoa simu Kali cheki.

Huawei watangaza rasmi kuja na mfumo endeshi (OS) wao mpya kwa ajili ya simu zao na kompyuta mpakato mwanzoni mwa mwaka 2020. Mkurugenzi mtendaji wa Huawei upande wa Consumer Business Group, Richard Yu, alisema mfumo endeshi wao mpya upo tayari kwa ajili ya simu na kompyuta, na utaanza kutumika katika kipindi cha robo ya nne ya mwaka huu (Q4) nchini China, ila kuanzia robo ya kwanza (Q1) na ya pili (Q2) ya mwaka 2020 ndipo utaachiwa kutumika rasmi kwa nchi zingine nje ya China. Mfumo endeshi huo utakuja na soko la app zake linaloitwa App Gallery mkabala kushindana na Google Playstore, Yu pia alisema kama Huawei watazuiwa kabisa kutumia mifumo endeshi kutoka Microsoft na Google basi hawatakuwa na njia nyingine zaidi ya kutumia mfumo endeshi wao huo mpya. Google walitangaza kusitisha huduma ya Android kwa Huawei, baada ya kampuni hiyo kuwekwa kwenye orodha ya 'Entity List' na serikali ya Marekani - Hii inamaana kampuni yoyote nchini Marekani ikitaka kufanya biashara na Huawei lazima ipate kibali kutoka serikalini. #andrewsoft #teknolojia #simu

No comments:

Post a Comment